Home » » UTAFITI::: Uingizwaji dawa holela ni dili la VIGOGO, Utafiti wa kimataifa waweka ''uchi'' ripoti ya utafiti...

UTAFITI::: Uingizwaji dawa holela ni dili la VIGOGO, Utafiti wa kimataifa waweka ''uchi'' ripoti ya utafiti...

Dar es Salaam. Utafiti uliochapishwa kwenye jarida la kimataifa unaonyesha kuwa mchakato wa mabadiliko ya sera ya uuzaji wa dawa za binadamu nchini, umegubikwa na ufisadi ukihusisha viongozi wa Serikali.
Jarida la Afya la Kimataifa linalochapishiwa nchini Uingereza, limechapisha utafiti huo likisema mabadiliko ya sera hiyo ambayo sasa imebadili mfumo uliokuwapo wa maduka ya dawa baridi za binadamu, kuwa ya dawa muhimu sasa ni janga linalozinyemelea afya za Watanzania.
Kwa mujibu wa jarida hilo hadi upitishwaji wa muswadwa wake bungeni, uliingiliwa na vigogo serikalini pamoja na wafanyabiashara wakubwa kwa malengo ya kujinufaisha.
Jarida hilo linaloitwa BMC Public Health toleo la mwezi huu, limechapisha ripoti hiyo wakati ambapo tayari Serikali imeanza kutekeleza sera hiyo kwa kubadili maduka ya dawa baridi kuwa maduka ya dawa muhimu ambapo yanatatawanywa hadi vijijini na yataruhusiwa kuuza baadhi ya dawa kali za magonjwa makubwa.
Hata hivyo, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imetoa msimamo wake ikisema inaichukulia ripoti hiyo kama ni maoni ambayo mtu yeyote anaweza akayatoa, na kwamba hawatarudi nyuma kwa kuwa wanajiamini mchakato ulifuata sheria na taratibu za nchi.
Yaliyomo kwenye ripoti
Ripoti hiyo inaonyesha kuwa utafiti ulifanyika kati ya mwaka 2011 na 2012, na kubaini kuwa kuundwa kwa sera hiyo, kulizingatia zaidi masilahi binafsi yaliyoandamana na msukumo wa kisiasa na kibinafsi.
Inaeleza sera hiyo haikuzingatia ufanisi wa kitaalamu wa huduma nzuri katika sekta ya afya bali kuweka wigo mpana ambao mtu yeyote mwenye fedha au anayeshawishika na biashara hiyo aweze kuwekeza bila kipingamizi.
Jarida hilo liliipa ripoti hiyo kichwa cha habari: “Mabadiliko ya sera kisekta: Ni kwa ajili ya ufanisi au kuweka wigo mpana ili kila anayevutiwa awekeze? Ni ripoti ya utafiti uliofanyika Tanzania kuhusu mabadiliko ya sera ya uuzaji wa dawa.”
Jambo hilo likatafsiriwa kuwa ni la hatari na ambalo Serikali inapaswa kuingilia kati ili kuepusha janga la kiafya linaloinyemelea jamii.
“Serikali inapaswa kuingilia kati na kupunguza ushawishi wa kisiasa kwa masilahi binafsi kwenye mambo ya kitaaluma,” inashauri sehemu ya taarifa hiyo ikionya:
“Kutoondoa tatizo hilo la udhibiti wa dawa kunaweza kusababisha madhara makubwa ya afya kwa umma.”
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan Tanzania Mpya untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Hisia za Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2013. Tanzania Mpya - All Rights Reserved
Template Modify by Hisia za Mwananchi
Proudly powered by Hisia