Home » » NIMRODI MKONO naye apinga serikali tatu, adai kuwa, una lengo la kutugawa kama kipindi cha ukoloni

NIMRODI MKONO naye apinga serikali tatu, adai kuwa, una lengo la kutugawa kama kipindi cha ukoloni

Mjadala unaoendelea kuhusu rasimu ya Katiba Mpya, unayagusa makundi mengi ya kijamii na watu binafsi, kila upande kwa namna yake.
Lakini sehemu kubwa ya mjadala huo imejikita katika muundo wa utawala wa nchi, ambapo rasimu hiyo iliyotolewa na Tume ya Marekebisho ya Katiba, imependekeza kuwapo serikali tatu. Pendekezo hilo, limechukua sehemu kubwa katika mjadala unaoihusu rasimu hiyo.
Mmoja wa watu ni Nimrodi Mkono, Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM) na mwanasheria aliyebobea katika tasnia hiyo kwa miongo kadhaa sasa.
Mkono, anajenga hoja yake juu ya msingi kwamba, Katiba inafaa kuwapo, lakini haipaswi kuwa jambo lenye uzito kiasi cha ‘kuteka’ mapokeo na nia chanya za viongozi waasisi katika nchi za Afrika, hususani kuhusu umoja wa nchi hizo na kupunguza wingi wa serikali zenye mamlaka kamili.
Ndiyo maana, Mkono anasema mfumo wa serikali tatu katika Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, utakuwa muendelezo wa mbinu za kikoloni, wenye lengo la kuwagawa wananchi na kutoa fursa pana ya uporaji wa rasilimali za nchi.
Hivyo anasema, kiongozi yeyote anayeutetea mfumo huo, hapaswi kuutumikia umma wa Tanzania, hasa katika nafasi ya Urais.
Kwa mujibu wa Mkono, Katiba si kitu kinachohitaji nguvu kubwa, badala yake nchi inaweza kuweka mambo ya msingi yan
ayopaswa kukubalikuwa, kufuatwa na kutekelezwa kama ilivyo kwa Uingereza.
“Wanaotaka serikali tatu, binafsi ninawaona kama wenye fikra mgando, hawayaishi mambo mema yaliyoasisiwa na viongozi katika nadharia ya kuwapo Afrika moja, tukagawanywa na wakoloni na sasa wanataka kuigawa Tanzania,” anasema.
Mkono anasema tangu wakati wa ukoloni, Waafrika walikuwa wamoja, wakitendewa uovu na wakoloni walioingia barani humo kwa lengo la kupora rasilimali zao.
“Sasa wanaotaka Tanzania igawanyike na kuwa na serikali tatu, wanafanya hivyo kutoa mianya ya wazungu kuendelea kupora rasilimali zetu, watu wa aina hiyo hawafai kuwa marais wa nchi hii,” alisema.
Mkono anasema hoja hiyo alitaka kuiwasilisha bungeni mjini Dodoma, lakini ikadhibitiwa kwa mujibu wa kanuni zinazotoa muda mfupi kwa Mbunge kuzungumza.
Hata hivyo, Mkono, anasema ili Tanzania ijiimarishe kwa umoja, amani, utulivu, maendeleo na ustawi wa jamii, inahitaji kubaki katika mfumo wa serikali moja na kuwa na kiongozi mkuu (Rais) anayesimamia maslahi ya umma pasipo mgawanyiko.
AWASHANGAA WARIOBA, SALIM
Mkono anasema, inashangaza kuona wajumbe wa Tume ya Marekebisho inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba, kuwasilisha pendekezo la serikali tatu, huku wakiwa na uelewa wa kihistoria kuhusu umoja wa kuwapo umoja barani Afrika.
Ingawa hakuwataja kwa majina, Mkono, akaisema wapo watu waliowahi kuwa katika kundi G55 lililoibua hoja ya kuwapo serikali ya Tanganyika, na sasa wanataka kuifanikisha azma hiyo kupitia Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Jaji Warioba, anatajwa kuwa miongoni mwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walioibua hoja ya Utanganyika mwaka 1994, wakati wa utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi, ambayo hata hivyo, ilizimwa kwa msaada wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Mkono, anasema pia kuwa katika tume ya Warioba, yumo mjumbe aliyewahi kuwa kiongozi wa juu katika Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), aliyetekeleza jukumu ya kuihubiri ‘Afrika moja’, lakini sasa ameingia katika orodha ya wanaotaka kuigawa Tanzania.
Mjumbe wa tume hiyo, Dk. Salim Ahmed Salim, alikuwa Katibu Mkuu wa sita wa OAU, ambaye kumbukumbu zinaonyesha aliifanya kazi hiyo kati ya Septemba 19, 1989 hadi Septemba 17, 2001.

From: nipashe jpili
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan Tanzania Mpya untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Hisia za Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2013. Tanzania Mpya - All Rights Reserved
Template Modify by Hisia za Mwananchi
Proudly powered by Hisia