Home » » BAKWATA sasa yamuunga mkono PONDA, yawaponda POLISI..........

BAKWATA sasa yamuunga mkono PONDA, yawaponda POLISI..........

 Baraza la waislamu Tanzania BAKWATA limeitaka serikali kuunda tume huru ya uchunguzi na kumtaka kamanda wa polisi mkoani Morogoro Faustine Shilogile kujiuzulu ili kupisha tume hiyo itakayoundwa kulifanyia uchunguzi madai ya tukio la katibu wa jumuia na taasisi za Kiislamu nchini shekhe Ponda Issa Ponda kupigwa risasi na polisi mkoani humo huku familia yake ikitoa msimamo wao kuhusiana na tukio hilo.
Msimamo huo wa BAKWATA umetolewa na sheikh mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum katika makao makuu ya mkoa ya baraza hilo na kuongeza kuwa licha ya Bakwata kutofautiana kifikra na Sheikh Ponda hawaungi mkono kwa namna yeyote ile tukio hilo la madai ya kupigwa risasi na polisi huku akilitaka jeshi la polisi nchini kujipanga upya katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kuepuka matumizi makubwa ya nguvu ikiwa ni pamoja na kutumia risasi za moto kwa raia kwa kuwa hali hiyo inachafua sura na amani ya nchi iliyopo hivi sasa na kuwataka wote waliohusika katika tukio hilo kuwajibishwa.
Sheikh Alhad ameonya kuwa endapo itathibitika pasi na shaka kuwa sheikh Ponda amedhuriwa kwa risasi ya moto na jeshi la polisi ni dhahiri kuwa mahusiano mema baina ya raia hasa wa jamii ya kiislamu na polisi yatakuwa ni ya mashaka.
Akizungumza na vyomba vya habari katika taasisi ya tiba ya mifupa na upasuaji wa mishipa ya fahamu, MOI meneja uhusiano wa MOI Juma Almas amekiri sheikh Ponda kulazwa hospitalini hapo na kwamba imekuwa ni vigumu kujua majeraha aliyo nayo yamesababishwa na kitu gani kwa kuwa majeruhi alifikishwa katika taasisi hiyo akiwa tayari ameshashonwa jeraha.
Katika taasisi ya tiba ya mifupa na upasuaji wa mishipa ya fahamu,moi alikolazwa sheikh ponda issa ponda ambapo itv imemtembelea na kuonana nae licha ya kutozungumza lolote msemaji wa familia hiyo amesema wanapata mashaka kutokana na kile alichokiita kuwa ni upotoshaji wa makusudi unaofanywa kuficha sababu za sheikh Ponda kuumizwa na kusema kile familia inachoamini kimemdhuru sheikh Ponda.
Katika eneo hilo la wodi alikolazwa sheikh Ponda kumeonekana uwepo wa ulinzi mkali ambapo ITV imeshuhudia askari kanzu pamoja na baadhi ya askari waliokuwa na silaha wakilinda eneo lote la wodi hiyo.
 
source ITV TZ
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan Tanzania Mpya untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Hisia za Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2013. Tanzania Mpya - All Rights Reserved
Template Modify by Hisia za Mwananchi
Proudly powered by Hisia