Home » » MALIMWENGU : Ni sahihi kupekua simu ya mwenza wako?

MALIMWENGU : Ni sahihi kupekua simu ya mwenza wako?

Katika mambo yaliyo magumu kwenye maisha kwa watu walio wengi, basi ni kupekuliwapekuliwa. Wapo wanawake ambao hudiriki hata kuwapekua simu za viganjani  za waume zao na kuweka miaka waliyozaliwa, ili ahakiki mumewe ana shilingi ngapi kwenye akaunti yake ya simu yaani Tigo-pesa, Mpesa au Airtel Money.
Swali la wiki hii liliuliza:
Utakuta mwanamke anapekua simu ya mumewe au mwanaume anapekua ya mkewe, pengine msichana anapekua simu ya mpenzi wake au mvulana anafanya hivyo. Kupekuliana simu ni sawa?
Wadau wa safu hii walijibu hivi:
Prosper Mallya, Moshi
Suala la kupekua simu ya mke wako au mume wako,  mie naona ni suala ambalo limeshakua kama ni mazoea, maana  nyingine ni kama ngozi yako ya mwili hapo ni uaminifu tu unahitajika.
Danny Chumu, Dar es Salaam
Kupekua pekua simu ya mpenzi wako siyo jambo jema hata kidogo inafaa kuaminiana tu wala sioni haja ya kupekua  katika simu ya mwenzi wako.
Ashura Amily, Kibaha
Kupekua simu ya mkeo/mumeo au mpenzi wako ni sawa hapo ndiyo mtaaminiana na mapenzi mliyokuwa nayo ni ya kweli unapata kujua tabia za mwenzi wako.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan Tanzania Mpya untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Hisia za Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2013. Tanzania Mpya - All Rights Reserved
Template Modify by Hisia za Mwananchi
Proudly powered by Hisia